MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mashine Kusaidia Uuzaji Vinywaji Bila Muuzaji
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mashine Kusaidia Uuzaji Vinywaji Bila Muuzaji
Habari

Mashine Kusaidia Uuzaji Vinywaji Bila Muuzaji

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Lyatuu
MHADHIRI mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) Kilavo Hassan amebuni mashine  kwa mfumo wa ‘ATM’ ambayo mtu anaweza kujihudumia mwenyewe.
 Amesema Hiyo inatokana na  kuweka urahisi wa ufanyaji wa biashara pasipo uwepo wa watu,ambapo  mbinu mpya na rahisi imebuniwa ambayo itafanya biashara kujiendesha kidigitali.
“Mashine hiyo inawezesha watu kujihudumia huku muuzaji akiwa na uwezo wa kufanya hadi biashara nne kupitia mashine moja pekee,”amesema.
Kila amesema mbinu hiyo inaweza kuwa ahueni kwa wauzaji wa vinywaji ikiwemo juisi, bia, maziwa au maji katika maeneo mbalimbali nchini.
Mashine hiyo ipo  katika maonyesho ya 49 ya biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayoendelea .
Amesema  Kwa sasa mtu atakuwa na uwezo wa kusimika mashine hizi katika maeneo mbalimbali analotaka kufanyia kazi na kuacha watu wajihudumie.
Amesema Mashine hiyo inampa mtu machaguo matatu kwa ajili ya kulipia, ya kwanza ni sarafu, ya pili ni noti na ya tatu ni lipa namba. Lipa namba ni rahisi zaidi kwa sababu unakuwa na uwezo wa kuangalia utendaji sa biashara zako moja ksa moja kupitia eneo alilopo.
Akielezea mashine hiyo inavyofanya kazi amesema, ili mtu aweze kuhudumiwa anatakiwa kuja na chombo chake cha kubebea kinywaji na maelekezo yote huwekwa.
“Tunaweka maelezo kuwa ukilipia kiasi kadhaa utapata ujazo kiasi gani kama ni kileo au kinyeaji baridi, mtu anakuwa anajua anahitaji chombo kikubwa kiasi gani ili aweze kupata ujazo wa bei anayohitaji,” amesema.
Amesema uwepo wa mashine hiyo pia utawezesha uuzaji wa vinywaji kidogokidogo hivyo kumfanya mtu kuwa na uwezo wa kumudu kwa gharama zake.
“Kama ni maziwa ya Sh500, au juisi au Kileo cha Sh500 mtu anaweza kujihudumia. Mashine hii huweza kuuza hadi bidhaa aina nne bila kuchanganyikana kwa sababu kila bidhaa itakuwa na koki yake maalumu ambayo ina maelekezo kuwa ukitaka maji utapata koki hii, maziwa koki hii, pombe koki hii,” amesema.
Amesema ndani yake, hufungwa matanki yenye ujazo kuendana na mahitaji ya mteja lakini yapo ya kuanzia lita 18 na huweza kuongezwa kulingana na mahitaji ya mteja.
“Mtu akihitaji hii bei hubadilika kulingana na mahitaji yake lakini huanzia Sh14 milioni,” amesema huku akisema hadi sasa wameshapokea oda za wateja mbalimbali.
Akizungumzia usalama wa uendeshaji wa biashara hiyo,  amesema mtu anaweza kuijengea kibanda cha nondo kama ambavyo inafanywa na wafanyabiashara wenye majokofu yanayokaa nje.

You Might Also Like

DART Toeni Fursa Kwa Watanzania Kuwekeza kwenye Mwendokasi -Mchengerwa

Rais Samia Azindua Makao Makuu Ya Mahakama Tanzania

SGR Kipande Cha Saba Na Nane kuanza kujengwa

Miaka 60 Mikumi na mapinduzi makubwa sekta ya utalii

China yatoa elimu ya ujenzi kwa wanafunzi Baobab

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tanzania Yafungua Milango Ya Biashara Na Jumuiya Ya Ulaya
Next Article VETA Yang’ara Sabasaba
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

MAIPAC Yagawa Makoti Ya Usalama Kwa Wanahabari Kuelekea Uchaguzi Mkuu.
Habari July 8, 2025
Watafiti Watumia Mbinu Mpya Kudhibiti Mdudu Kantangaze Kwenye Nyanya Bila Viuatilifu
Habari July 8, 2025
PSSSF Itaendelea Kuwekeza Kwenye Maeneo Salama Yenye Tija
Habari July 8, 2025
Taasisi Za Umma Zasisitizwa Kuzingatia ubora Wa Mikataba Katika Utekelezaji Wa Majukumu Yao
Habari July 8, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?