MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Washauri Serikali Kutumia Fedha Za Miradi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Washauri Serikali Kutumia Fedha Za Miradi
Habari

Washauri Serikali Kutumia Fedha Za Miradi

Author
By Author
Share
4 Min Read
Na Danson Kaijage
DODOMA: SERIKALI imetakiwa kufuatilia kwa ukaribu fedha zinazotengwa kwa ajili ya  miradi ya maendeleo ili iendane na thamani halisi ya fedha inayotengwa.
Hayo yamebainishwa na washiriki walioshiriki katika mdahalo ulioandaliwa na mradi wa maendeleo wa Acrionaid, kuangalia namna nchi inavyoweza kuwekeza bila kuongeza fedha za mikopo kutoka mataifa ya nje na kuongeza madeni kwa taifa.
 Mmoja wa wakulima wa zao la Zabibu wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma, Nuru Said amesema licha ya Serikali kukopa fedha kwa ajili ya maendeleo, bado kuna fedha ambayo haitumiki ipasavyo katika kuleta tija ya mradi lengwa.
Nuru amesema imefikia hatua ukaguzi pekee wa miradi unatumia fedha nyingi kuliko mradi mwenyewe jambo ambalo linasababisha kuongeza deni kubwa la fedha ya mkopo kwani Serikali haipo makini katika kufuatilia thamani halisi fedha zinazotengwa kwa ajili ya miradi husika.
“Mimi ni Mkulima wa zabibu na tulipewa mradi wa kilimo hicho lakini cha kushangaza waliokuja kukagua wanaeleza kutumia lita 60 za mafuta na ilikuwa ijengwe choo cha matundu mawili ya choo lakini limejengwa tundu moja kwa bajeti hiyo hiyo na hakuna ufuatiliaji wowote,” amesema.
Amesema kwa Serikali kutofuatilia matumizi bora ya fedha inayotengwa kwa ajili ya kuendeleza miradi ya maendeleo ni mwendelezo wa kukuza deni la taifa.
Mratibu wa Actionaid kutoka Zanzibar, Bakari Khamis Said  amesema  wameona ni muafaka kuitisha mkutano kujadili namna yakushauri  kufadhili maendeleo kwa kutumia vyanzo vya ndani.
Amesema  kumekuwa na changamoto ya uchumi kukua  lakini mahitaji ya kimaendeleo katika masuala ya miradi inakua kila siku na inahitajika kutafuta rasimali za kuendana na maendeleo hayo.
Amesema kwa sasa mashirika ya kimarekani yamesitisha misaada imekuwa ikiathiri maendeleo hivyo wanaweza kuhamasisha watanzania kutafuta rasilimali za ndani kwa kuimarisha usimamizi wa kodi na  mapato yasiyo ya kodi kuimarisha usimamizi wa mapato.
Hata hivyo ameeleza kuwa kama serikali itaimarisha   usimamizi wa matumzi yasiyo ya lazima,kupunguza posho serikalini , kupunguza gharama za safari inaweza kujikuta haijiingizi katika mikopo ya kibenki ambayo ni ya kibiashara zaidi.
Naye Program Meneja wa Mtandao wa Madeni, Boniface Komba amesema kumekuwa na ukuaji wa deni la serikali lakini suala la kukopa halizuiliki.
Hata hivyo amesema kwa sasa ugharamiaji deni umekuwa ni mkubwa na linaweza sababisha  athari kwa huduma za kiafya kutokana na kulipa deni kwa dola licha ya  deni kuwa ni himilivu.
Ameeleza pamoja na yote,  serikali iwe na nidhamu ya fedha katika ukopaji  na kusimamia matumizi kwani baadhi ya ripoti ya  Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG), imeonyesha kuwepo na  mianya ya upotevu wa fedha.
Samwel Mkwata kutoka Policy Forum and Policy amesema ameangalia nchi namna inavyoweza kuwekeza kwenye maendeleo ya nchi.
Amesema kutokana na  misaada kuendelea kupungua nchi ya Tanzania inaweza kujiendesha kwa asilimia kubwa kupitia mabadiliko ya kikodi.
Amesema kuwa katika majadiliano ya kuimarisha uchumi wa nchi ya Tanzania   wanaishauri serikali kuwekeza zaidi ili mwisho wa siku wasitegemee misaada toka nje.

You Might Also Like

Watafiti Wa Mimea Vamizi Watua Serengeti

TIB Yaanda Mkakati Kabambe Wanawake Kuchangamkia Fursa

Kasi Ya Kusambaza Umeme Kwenye Vitongoji Yaanza-Kapinga

TAKUKURU kuelimisha madhara ya rushwa wakati wa uchaguzi

TPHPA, KEM Wasaini Hati Ya Makubaliano Udhibiti Viuatilifu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Rais Samia Azungumzia Mafanikio Ya Nishati Nchini
Next Article Madini Yaweka Rekodi Makusanyo Ya Maduhuli
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

VETA Dodoma Waleta Mashine Kurahisishia Upekechuaji Wa Alzeti
Habari July 3, 2025
VETA Shinyanga Waja Na Mafunzo Ya Saluni, Mapambo, Urembo
Habari July 3, 2025
UDSM Yaja Na Bajaji Inayotumia Maji Na Mafuta
Habari July 3, 2025
Bodi ya Bima ya Amana Yatoa  Bil 9.07 , Fidia Kwa Wateja Wa Benki Saba   Zilizofilisika
Habari July 3, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?