MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Uongozi CHADEMA Kanda Ya Kati Upo Imara
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Uongozi CHADEMA Kanda Ya Kati Upo Imara
Habari

Uongozi CHADEMA Kanda Ya Kati Upo Imara

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Danson Kaijage.
UONGOZI wa Chama cha Demokrasia na  Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Kati umesema nafasi zilizoachwa na viongozi walioondoka, zitazibwa siku za karibuni.
Aidha uongozi huo umewatakia heri wanachama wote walioondoka katika chama hicho.
Hayo yameelezwa na Katibu Mtendaji wa chama hicho Kanda ya Kati,  Ashura Masoud alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya mwenendo wa kisiasa katika chama hicho.
Amesema suala la mwanachama kuhama chama na kujiunga na chama kingine ni jambo la kawaida na ni la kidemokrasia hivyo kila anayetaka kuondoka CHADEMA na kujiunga na chama kingine ruksa kwa kuwa chama hicho, siyo gereza la kuwafungia wanachama.
“CHADEMA ni taasisi na CHADEMA ni bora kuliko mwanachama hivyo kuna watu wameondoka ndani ya chama kwa kushindwa kufuata misingi ya chama chetu, CHADEMA inawatakia heri na wanatakiwa kujua kuwa CHADEMA ni imara sana.
“Tumeshuhudia uchaguzi wa 2019 wa Serikali za Mitaa ulivyokuwa wa ovyo,tumeshuhudia uchaguzi wa 2020 ulivyokuwa wa ovyo zaidi na sasa tunasema kama hakuna Tume Huru ya uchaguzi hakuna uchaguzi hatuwezi kuingia kwenye uchaguzi ili watu waumizwe kutokana na mifumo ya ovyo ya uchaguzi,” amesema.
Pia amesema chama hicho kimejaa  hazina ya viongozi makini ambao wanaweza kuongoza tena kwa uhakika zaidi hivyo wale wanaoondoka kwa visingizio mbalimbali wanatakiwa kupuuzwa ili shughuli ya kimapambano iendelee.
Amesema inashangaza kusikia mwanachama aliyehama au anayehama akidai kuwa Chadema imepoteza misingi yake wakati kashindwa kusimamia misingi,  hiyo inatokana na baadhi ya waliokuwa wanachama kutokuwa waumini wa chama bali ni waumini wa mtu.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Dodoma Dkt. Stevine Karashani amesema inawezekanaje kiongozi ndani ya chama mwenye nafasi ya uongozi akadai kuwa chama hakina maono wakati yeye hupo ndani ya uongozi.
Amesema  wapo waliokuwa wanachama ambao wamelelewa na chama hicho hadi kusafirishwa ughaibuni kwa ajili ya kupatiwa mafunzo lakini leo wanadai kuwa chama hakina maono hiyo ni aibu kwao kwani sasa wanatafuta kukubalika kwa nguvu.

You Might Also Like

Posta Yaleta   Usafiri Wa Kitalii Ndani Ya Sabasaba

November 8, 2024

SUA Yawafikia Wafugaji Wa Ng’ombe Wa Maziwa Kwa Tiba Mbadala Ya Homa Ya Kiwele

Rasmi Leo DSM Kuanza Biashara Saa 24

LHRC Kushirikiana  Na JOWUTA Kuwajengea Uwezo Wanahabari Katika Masuala Ya Haki Zao Na Sheria Za Kazi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Msisubiri Kupewa Amri, Ufanyaji Usafi Kwenye Maeneo Yenu – Lugendo
Next Article Shen Zhiying: Mkongwe Aliyeanzisha Kozi Ya Kiswahili Nchini China
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Serikali Yazindua Mafunzo Ya Mtandao Ya Afya Moja
Habari July 16, 2025
Watu Zaidi Ya 3500 Wapatiwa Huduma Ya Kisheria Wizara Ya Katiba Na Sheria
Habari July 16, 2025
Ubunifu Na Kufanya Tafiti Kwawezesha UDOM Kupokea Tuzo
Habari July 16, 2025
Utafiti Wa Nguvu Kazi, Mapato Ya Kaya Kutoa Taswira Mpya Ya Maendeleo
Habari July 15, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?