MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: VETA Yapaa Miaka Minne Ya Rais Samia
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > VETA Yapaa Miaka Minne Ya Rais Samia
Habari

VETA Yapaa Miaka Minne Ya Rais Samia

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Danson Kaijage

DODOMA: SERIKALI imetumia Sh. Bilioni 94.5 kwa ajili ya ujenzi wa vyuo 33 vya ufundi stadi, kati ya hivyo 29 vikiwa vya wilaya na vinne vya mkoa.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Anthony Kasore amesema hayo alipokuwa akielezea mafanikio ya mamlaka hiyo katika kipindi cha miaka minne  ya Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan, kuanzia 2021 hadi 2024.

Kasore amesema serikali pia ilitenga Sh. Bilioni 103 kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya ujenzi wa vyuo vipya 64 vya Wilaya na kimoja cha Mkoa wa Songwe, ambavyo vitachangia ongezeko la udahili wa wanafunzi 89,700.

Amesema kwa sasa VETA ina vyuo 80 hivyo mwishoni mwa mwaka huu 2025 vyuo vinavyojengwa vinatarajiwa kukamlika na kuwezesha kuwepo kwa vyuo 145 ambavyo vitakuwa mkombozi kwa vijana na watu wazima wanaotarajiwa kustaafu.

Akielezea mafanikio ya Mamlaka hiyo, amesema Serikali kupitia VETA imefanya upanuzi wa miundombinu  ya kutolea elimu na mafunzo ya ufundi stadi nchini kwa kutoa fedha ili kuongeza majengo mapya na ukarabati wa majengo ya zamani, kuweka mazingira wezeshi ya kukuza ubora wa mafunzo na kuongeza fursa za udahili katika vyuo vya VETA.

Akizungumzia eneo la upanuzi na uboreshaji wa miundombinu, amesema kipindi cha miaka minne Serikali imetoa kiasi cha Sh. Bilioni 14.2, ambazo zimewezesha uboreshaji na upanuzi wa miundombinu ya vyuo.

Vyuo hivyo ni chuo cha Newala, Ngorongoro, Moshi, Dar es Salaam (Changombe), Kipawa, Mtwara, Mwanza, Mikumi, Karagwe, Chuo cha Ualimu wa Ufundi Stadi Morogoro (MVTTC) Kihonda, Nkasi, Nyamidaho, Kanadi, Ileje, Namtumbo, Mabalanga, Gorowa, Arusha na Busokelo.

Kuhusu uongezekaji wa udahili na uhuishaji wa mitaala amesema katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya sita, jumla ya vijana 295,175 wamedahiliwa katika vyuo vya VETA katika kozi za muda mrefu na muda mfupi.

Kuhusu urasimishaji wa ujuzi uliopatikana nje ya mfumo rasmi wa mafunzo amesema kuwa kupitia Mpango wa Utambuzi na Urasimishaji ujuzi  uliopatikana nje ya mfumo rasmi, katika kipindi cha Mwaka 2021 hadi 2025, jumla ya wanagenzi 5,175 walitambuliwa na kurasimishiwa ujuzi wao.

Amesema kati ya yao wanagenzi 1,164, walikuwa wanaoshiriki miradi ya kimkakati ya Ujenzi wa Reli ya Mwendokasi (SGR) na Bwawa la la Umeme la Julius Nyerere (JNHPP) na 214 wapo kwenye vyuo vya kurekebisha tabia  ambao ni wafungwa katika Magereza ya Ukonga, Arusha na Morogoro.

 

You Might Also Like

Kijiji Cha Nzinga Kibaoni Kilwa Chapata Umeme

Wamiliki Migodi Wapewa Siku 30 Kufanya Usajili

BMT Yaleta Kicheko Kwenye Michezo

Lugendo Awataka Wananchi Kujenga Tabia Ya Kufanya Usafi

Baraza La Madiwani Lampongeza Rais Samia Kwa Utekelezaji Wa Ilani

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Rais Samia ametekeleza kwa vitendo falsafa ‘kazi iendelee’
Next Article Profesa Kabudi Atoa Maagizo Mazito Bodi Ya Ithibati Ya Waandishi Wa Habari
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Miaka Minne Ya Samia Na Sekta Ya Elimu
Habari May 28, 2025
Chalamila Atoa Wiki Mbili Wafanyabiashara Ndogo Ndogo Kufungua Njia Kariakoo
Habari May 28, 2025
Mtanda Akagua Maendeleo Ya Mradi YA Hoteli Ya Nyota Tano Ya NSSF
Habari May 27, 2025
UDSM  Kujenga Jengo La Kisasa La Bil 8.3
Habari May 27, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?