Na Lucy Lyatuu
WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni(BRELA). Umekuja na mfumo mpya ulioboreshwa ‘Brela Online Service’ ambao umeunganisha mifumo yote inayotolewa na Brela.
Akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba, Ofisa Leseni kutoka BRELA Sweetness Madata amesema mfumo huo umeanza kutumika mwezi Machi 2026.
Amesema kuwa mfumo huo umeweza kurahisha utendaji kazi katika shughuli za usajili kutokana na umaalum wake wa kuunganisha mifumo yote inayotoa huduma hapo.
Amefafanua kuwa mfumo huo wa BOS unasajili makampuni, utoaji wa leseni wa biashara kundi A, usajili wa viwanda.
Pia amewataka wahitaji wafike katika banda hilo ili waweze kupata huduma mbalimbali kwa urahisi papo kwa papo hakuna mzunguko.

