MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Daktari: Saratani ya Matiti Inazuilika, Inatibika
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Daktari: Saratani ya Matiti Inazuilika, Inatibika
Habari

Daktari: Saratani ya Matiti Inazuilika, Inatibika

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: DAKTARI Bingwa wa Magonjwa ya Saratani kutoka Hospitali ya Ocean Road, Dkt. Faraja Kiwanga, amesema mwezi huu wa Oktoba ni wa kuhamasisha uelewa kuhusu ugonjwa wa saratani ya matiti, ambao unaweza kuzuilika na kutibika iwapo utagunduliwa mapema.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, katika mafunzo yaliyoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), kuongeza uelewa kwa wanahabari kuhusu ugonjwa huo, Dkt. Kiwanga amesema saratani hutokea pale chembe hai za mwili zinapobadilika tabia zake za kawaida na kuanza kukua kwa kasi isiyo ya kawaida.
Amesema kwa sasa kuna zaidi ya aina 100 za saratani, ambazo huathiri watu wa rika zote wakiwemo watoto na watu wazima.
Kwa mujibu wa takwimu za hivi karibuni, kila mwaka watu zaidi ya milioni 11 duniani hugundulika na saratani, huku milioni tisa wakipoteza maisha, na zaidi ya milioni 43 wakiishi na ugonjwa huo.
Habari Picha 10185
Dkt. Kiwanga amesema nchini Tanzania, kwa kila watu 100,000, takriban wagonjwa 76 hugundulika na saratani, huku wagonjwa wapya 42,000 wakirekodiwa kila mwaka na takribani 28,000 wakifariki dunia kutokana na maradhi hayo.
Amesema changamoto kubwa ni wagonjwa wengi kufika hospitalini kwa kuchelewa, ambapo asilimia 75 ya wagonjwa hufika wakiwa katika hatua za mwisho za ugonjwa huo.
Kwa upande wa wanaume, saratani zinazoongoza ni za tezi dume, utumbo mkubwa na mdogo, huku kwa wanawake saratani ya mlango wa kizazi ikiongoza kwa asilimia 47, ikifuatiwa na saratani ya matiti (asilimia 16) na saratani ya koo.
Ametaja visababishi vinavyoweza kuzuilika kuwa ni pamoja na mtindo wa maisha usiofaa, ulaji wa vyakula vilivyokaa muda mrefu na kuota ukungu kama karanga na korosho, unene uliokithiri, matumizi ya tumbaku na pombe kupita kiasi, kutofanya mazoezi, na athari za kemikali za viwandani.
Dkt. Kiwanga amesema kwa wanawake, vichocheo vya saratani ya matiti ni pamoja na kuanza hedhi mapema, kuchelewa kukoma hedhi, kutokuzaa au kuzaa kwa umri mkubwa, kutonyonyesha, unene uliopitiliza, na matumizi ya pombe kupita kiasi.
Dalili kuu za ugonjwa huo ni uvimbe kwenye titi au kwapa, na amewataka wananchi kufika hospitalini mapema pindi wanapogundua mabadiliko yoyote.
Akimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji TAMWA,  Dkt. Rose Reuben, Meneja wa Mipango Mkakati Sylivia Daulinge,  amesema mwezi huu Oktoba ni muhimu kwa ajili ya kuelimisha jamii na kuwaenzi wote waliopitia changamoto ya saratani.
Amesema waandishi wa habari wana wajibu mkubwa wa kutumia kalamu zao kueneza elimu na kuongeza uelewa wa jamii kuhusu ugonjwa huo, huku akishukuru Hospitali ya Ocean Road kwa ushirikiano na utayari wao katika kutoa huduma bora kwa wagonjwa wa saratani.

You Might Also Like

Dar Sasa Kufanya Biashara Saa 24, Kuanza Februari 22 Mwaka Huu

Brela Yatoa Huduma Zote Za Usajili Katika Maonesho Ya Teknolojia Ya Madini Geita

Mitambo 10 Ya Uchimbaji Madini Yenye Thamani Ya Bilioni 10 Yazinduliwa

Ujenzi Miundombinu ya Kuongeza Udahili kipaumbele Cha Serikali

TRC Yawatoa Hofu Wasafirishaji Mizigo Kwa Malori

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Kituo Cha Umahiri Cha Upandikizaji Figo, Mafunzo, Kujengwa Hospitali Ya Benjamin Mkapa
Next Article Shibuda: WanaMaswa jitokezeni kupiga kura bila woga
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Wananchi wahamasishwa kuandika historia mpya kupitia kura
Habari October 25, 2025
Shibuda: WanaMaswa jitokezeni kupiga kura bila woga
Habari October 25, 2025
Kituo Cha Umahiri Cha Upandikizaji Figo, Mafunzo, Kujengwa Hospitali Ya Benjamin Mkapa
Habari October 24, 2025
Mwalim: Mchagueni Mwalimu Wangu Wa Siasa Shibuda
Habari October 24, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?