MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Daktari: Saratani ya Matiti Inazuilika, Inatibika
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Daktari: Saratani ya Matiti Inazuilika, Inatibika
Habari

Daktari: Saratani ya Matiti Inazuilika, Inatibika

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: DAKTARI Bingwa wa Magonjwa ya Saratani kutoka Hospitali ya Ocean Road, Dkt. Faraja Kiwanga, amesema mwezi huu wa Oktoba ni wa kuhamasisha uelewa kuhusu ugonjwa wa saratani ya matiti, ambao unaweza kuzuilika na kutibika iwapo utagunduliwa mapema.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, katika mafunzo yaliyoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), kuongeza uelewa kwa wanahabari kuhusu ugonjwa huo, Dkt. Kiwanga amesema saratani hutokea pale chembe hai za mwili zinapobadilika tabia zake za kawaida na kuanza kukua kwa kasi isiyo ya kawaida.
Amesema kwa sasa kuna zaidi ya aina 100 za saratani, ambazo huathiri watu wa rika zote wakiwemo watoto na watu wazima.
Kwa mujibu wa takwimu za hivi karibuni, kila mwaka watu zaidi ya milioni 11 duniani hugundulika na saratani, huku milioni tisa wakipoteza maisha, na zaidi ya milioni 43 wakiishi na ugonjwa huo.
Habari Picha 10185
Dkt. Kiwanga amesema nchini Tanzania, kwa kila watu 100,000, takriban wagonjwa 76 hugundulika na saratani, huku wagonjwa wapya 42,000 wakirekodiwa kila mwaka na takribani 28,000 wakifariki dunia kutokana na maradhi hayo.
Amesema changamoto kubwa ni wagonjwa wengi kufika hospitalini kwa kuchelewa, ambapo asilimia 75 ya wagonjwa hufika wakiwa katika hatua za mwisho za ugonjwa huo.
Kwa upande wa wanaume, saratani zinazoongoza ni za tezi dume, utumbo mkubwa na mdogo, huku kwa wanawake saratani ya mlango wa kizazi ikiongoza kwa asilimia 47, ikifuatiwa na saratani ya matiti (asilimia 16) na saratani ya koo.
Ametaja visababishi vinavyoweza kuzuilika kuwa ni pamoja na mtindo wa maisha usiofaa, ulaji wa vyakula vilivyokaa muda mrefu na kuota ukungu kama karanga na korosho, unene uliokithiri, matumizi ya tumbaku na pombe kupita kiasi, kutofanya mazoezi, na athari za kemikali za viwandani.
Dkt. Kiwanga amesema kwa wanawake, vichocheo vya saratani ya matiti ni pamoja na kuanza hedhi mapema, kuchelewa kukoma hedhi, kutokuzaa au kuzaa kwa umri mkubwa, kutonyonyesha, unene uliopitiliza, na matumizi ya pombe kupita kiasi.
Dalili kuu za ugonjwa huo ni uvimbe kwenye titi au kwapa, na amewataka wananchi kufika hospitalini mapema pindi wanapogundua mabadiliko yoyote.
Akimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji TAMWA,  Dkt. Rose Reuben, Meneja wa Mipango Mkakati Sylivia Daulinge,  amesema mwezi huu Oktoba ni muhimu kwa ajili ya kuelimisha jamii na kuwaenzi wote waliopitia changamoto ya saratani.
Amesema waandishi wa habari wana wajibu mkubwa wa kutumia kalamu zao kueneza elimu na kuongeza uelewa wa jamii kuhusu ugonjwa huo, huku akishukuru Hospitali ya Ocean Road kwa ushirikiano na utayari wao katika kutoa huduma bora kwa wagonjwa wa saratani.

You Might Also Like

LATRA CCC Yatoa Angalizo Uhitaji Mkubwa Wa Wasafiri Mwisho Wa Mwaka

Tanzania Yatumia Wiki Ya Nishari India Kunadi Vitalu Vya Mafuta Na Gesi Asilia

ATCL Yaanzisha Safari Za Moja Kwa Moja, Dubai Na Zanzibar

Chanzo Cha Bunge Kuridhia Hoja Ya Wanaojifungua Njiti, Kilianzia Hapa

Madereva Mabasi YA Kukodi Waitwa LATRA Kabla YA Januari 12, Mwaka Huu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Kituo Cha Umahiri Cha Upandikizaji Figo, Mafunzo, Kujengwa Hospitali Ya Benjamin Mkapa
Next Article Shibuda: WanaMaswa jitokezeni kupiga kura bila woga
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Kijaji: Huduma ya Kudungwa na Nyuki Kuongeza Kinga Yavutia Bungeni
Habari May 15, 2026
Serikali  Kutumia Fursa  ya AFCON,  Miss World Na IPU Kukuza Utalii Nchini
Habari May 15, 2026
TFS Yavunja Rekodi Utalii Wa Misitu,Mapato Yapaa Kwa Asilimia 43
Habari May 15, 2026
Serikali Kuimarisha Uvuvi Bahari Kuu Kupitia TAFICO
Habari May 14, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?