MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: UDOM Yatafiti Dawa za Malaria, Vidonda vya Tumbo, Kisukari Kutoka Mimea ya Asili
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > UDOM Yatafiti Dawa za Malaria, Vidonda vya Tumbo, Kisukari Kutoka Mimea ya Asili
Habari

UDOM Yatafiti Dawa za Malaria, Vidonda vya Tumbo, Kisukari Kutoka Mimea ya Asili

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimewasilisha bunifu mpya ya dawa za asili kwa ajili ya matibabu ya malaria, vidonda vya tumbo, na ugonjwa wa kisukari.

Utafiti wa dawa hizo umefanywa kuunga mkono juhudi za kitaifa za kutatua changamoto za kiafya kwa njia endelevu na salama.

Akizungumza katika banda la UDOM kwenye maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara yajulikanayo kama Sabasaba, Mtafiti wa Mradi huo ambaye ni mhadhiri chuoni hapo, Dismas Tullo amesema utafiti huo unalenga kutumia rasilimali za asili zilizopo nchini hasa mimea tiba kuandaa dawa mbadala salama kwa magonjwa yanayoathiri watanzania kwa kiwango kikubwa.

“Tumegundua kuwa mimea mingi ambayo inatupwa au haithaminiwi ina uwezo mkubwa wa kiafya. Ndiyo maana tumeamua kufanya tafiti na kuzalisha dawa ambazo zitatatua changamoto halisi katika jamii,” amesema.

Akielezea dawa ya kisukari ya Gymerine amesema inalenga kupunguza kiwango cha sukari mwilini kwa wagonjwa wa kisukari.

Amesema dawa hiyo imefanyiwa majaribio ya awali katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), ambapo baadhi ya wagonjwa waliotumia dawa hiyo wameonyesha maendeleo chanya ya kiafya.

Kwa upande wa matibabu ya vidonda vya tumbo, UDOM imebuni dawa iitwayo Ulcerexia, ambayo kwa sasa ipo kwenye hatua ya majaribio ya kitabibu.

Wagonjwa wa awali waliotumia dawa hiyo walionyesha hali nzuri ya kupona, huku tafiti zaidi zikiendelea kuthibitisha usalama na ufanisi wake kwa matumizi ya binadamu.

Amesema katika mapambano dhidi ya ugonjwa sugu wa malaria, chuo hicho kimebuni dawa mpya iitwayo Malaherb, ambayo imeundwa kwa kutumia mimea ya asili yenye uwezo wa kupambana na vimelea vya malaria.

Tofauti na dawa mseto inayotumika kwa sasa na kuhitaji vidonge vingi kwa dozi moja, Malaherb imetengenezwa kwa kuzingatia urahisi wa matumizi kwa mgonjwa.

“Wagonjwa wengi wa malaria wanashindwa kumaliza dozi ya dawa mseto kwa sababu ya idadi kubwa ya vidonge.

“Hali hiyo hupelekea ugonjwa kurudi au kusababisha madhara mengine kama matatizo ya figo. Malaherb ni dozi rafiki, rahisi kutumia, na isiyo na madhara ya sumu,” alisema Tullo.

Mbali na dawa hizo, Tullo alibainisha kuwa chuo hicho pia kimebuni bidhaa za lishe maalum kwa wagonjwa wa kisukari, wagonjwa wa ini, watoto wenye utapiamlo pamoja na watu wanaoishi na VVU. Bidhaa hizo zinalenga kuboresha kinga ya mwili na kusaidia katika kuimarisha afya kwa kundi hilo maalum la watu.

“Tunachokifanya ni kuleta sayansi kwenye tiba za asili kwa kuhakikisha kuwa bidhaa tunazozalisha ni salama, zinafanyiwa majaribio na zina viwango vya kitaalamu vinavyokubalika,” amesema.

You Might Also Like

Tanzania Kidedea Tuzo Ya Mashindano Ya Kimataifa  Usalama wa Barabara

Ndizi, Mchele, Mafuta Vyapanda Bei

Sera mpya ya viwanda kuzinduliwa

Dkt. Biteko Aahidi Kuendeleza Miradi Mikubwa Bugelenga

Kamati YA Siasa Yaendelea Kukagua Miradi Ya Maendeleo Temeke

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wanafunzi UDOM Wavumbua Mafuta ya Asili Kutoka Mabaki ya Zabibu
Next Article Wananchi Waelimishwe Kuhusu Utendaji wa Kamati za Maadili za Maofisa wa Mahakama
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?