MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Yapambana Kutokomeza Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Yapambana Kutokomeza Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele
Habari

Serikali Yapambana Kutokomeza Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: SERIKALI imetumia Sh. Bilioni 38.7 kwa ajili ya kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa ajili ya ununuzi, ugomboaji, utunzaji na usambazaji wa shehena za dawa, vifaa tiba na vitendanishi.
Waziri wa Afya Jenista Mhagama amesema leo Januari 30, 2025 katika kuadhimisha Kilele cha Siku ya Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele duniani.
“Hapa nchini Wizara kupitia Mpango wa Taifa wa Kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele inajihusisha zaidi na kudhibiti magonjwa matano ambayo ni matende na mabusha, trakoma, usubi, kichocho na minyoo.
“Kwa kuanzia Novemba hadi Disemba mwaka jana 2024. Halmashauri 130 zilifanya zoezi la kumezesha kingatiba za ugonjwa wa kichocho na minyoo ya tumbo,” amesema.
Amesema magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele duniani yapo zaidi ya 21, ambayo husababishwa na vimelea mbalimbali ikiwa ni pamoja na minyoo, bacteria, virusi na fangasi.
Amesema udhibiti wa magonjwa hayo ni kwa kufanya kampeni za ugawaji kingatiba kwa walengwa kulingana na ugonjwa husika.
“Makundi ya walengwa hao ni pamoja na jamii nzima, watoto wenye umri wa kwenda shule kuanzia miaka mitano hadi 14 na makundi maalum yaliyo katika mazingira hatarishi dhidi ya magonjwa hayo,” amesema.
Amesema Serikali imewekeza kwenye magonjwa hayo kwa kushirikiana na wadau imeweza kupata fedha pamoja na dawa za kutibu na kukinga magonjwa hayo hapa nchini.
“Aidha, Serikali kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali kwa mwaka 2024 tumeweza kutoa dawa za kingatiba za kudhibiti na kutokomeza magonjwa hayo kama ifuatavyo.
“Watu 257,358 kati ya 265,217 walipatiwa kingatiba za kutokomeza ugonjwa wa matende na mabusha kutoka kwenye Halmashauri za Mtama na Mtwara

Mikindani sawa na asilimia 97,.
“Watu milioni 5,462,851 kati ya 6,447,157
kutoka katika halmashauri 24 walipatiwa kingatiba ya ugonjwa wa Usubi sawa na asilimia 85, watu milioni 1,603,425 kati ya 1,967,143 kutoka Halmashauri saba za Ngorongoro DC, Monduli DC, Longido DC, Kiteto
DC, Simanjiro DC, Mpwapwa DC na Kalambo DC, walipatiwa kingatiba za ugonjwa wa trakoma,” amesema.
Amesema watoto wenye umri wa kwenda
shule yaani umri wa miaka 5 hadi 14 , 9,896,694 walilengwa kupatiwa huduma ya
kingatiba kwa ugonjwa wa minyoo ya tumbo ambapo hadi kufikia Disemba 2024 Watoto 8,676,234 sawa na asilimia 88 walimeza kingatiba.
Aidha, kwa ugonjwa wa kichocho walengwa wa kumeza kingatiba walikuwa 8,145,947 kati ya hao watoto 6,289,884 sawa na asilimia 77 walimeza
Kingatiba tajwa.
Walengwa hawa walifikiwa katika Halmashauri 171 sawa na asilimia 93 ya Halmashauri zote.
“Serikali kwa kushirikiana na wadau hutoa huduma kwa wananchi ambao tayari wamepata athari za magonjwa hayo ikiwemo upasuaji kwa watu wenye
tatizo la ugonjwa wa mabusha ambapo kwa mwaka 2024 watu wapatao 1,084 wamepatiwa huduma ya upasuaji,
“Na takriban wagonjwa 2,412 sawa na
asilimia 67 ya matarajio wenye tatizo la Vikope wamerekebishwa kope bila
malipo.,” amesema.
Amesema Miongoni mwa malengo ya Serikali  ni kuendelea kutumia rasilimali chache zilizopo katika kudhibiti magonjwa yanayowasumbua wananchi wake.

You Might Also Like

Dar es Salaam Kuunda Kamati Ya Kupitia Majengo Chakavu

Bodi ya mkonge kutoa ajira kwa watu 10,000 ifukapo 2030

Bajeti ya TUGHE 2025 Yaidhinishwa

TASU yaiomba serikali inunue kutoa ajira kwa mabaharia

Rais Mwinyi Kuzindua Maabara Nguvu Za Atomi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article RC Chalamila Ataka Reli Za Ndani Ya Mkoa Kusafirisha Abiria, Kupunguza Msongamano
Next Article Kamishna TRA Atua Kwa Malasusa Kushirikiana Elimu Kwa Mlipa Kodi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?