MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Rafiki Planter’Teknolojia Rahisi, Tija Kubwa”
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Rafiki Planter’Teknolojia Rahisi, Tija Kubwa”
Habari

Rafiki Planter’Teknolojia Rahisi, Tija Kubwa”

Author
By Author
Share
4 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: MASHINE mpya ya kupandia ya ‘ Rafiki Planter’ iliyobuniwa na watafiti wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kituo cha Ukirigulu mkoani Mwanza, inaleta mapinduzi ya kweli mashambani hivyo kuwawezesha wakulima kutumia muda mchache wawapo shambani.

Akiwa kwenye maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara yajulikanayo kama Sabasaba, Mtafiti kutoka TARI Ukiliguru, Dauson Malela ameielezea mashine hiyo kuwa ni ndogo, nyepesi na rahisi kutumia, imeundwa mahsusi kuwasaidia wakulima kupanda mazao kwa haraka, ufanisi, na kwa gharama nafuu.

Amesema mashine hiyo imeundwa kwa mfumo unaofanana na boda boda au bajaji hivyo Rafiki Planter ni chachu ya kuwavutia vijana kuingia kwenye kilimo chenye tija.

Amesema mashine hiyo inayotumia petroli lita moja kwa ekari moja, ina uwezo wa kupanda mazao kama mahindi, pamba na alizeti kwa kutumia saa moja tu kumaliza ekari moja.

“Tofauti na matumizi ya jembe la mkono yanayohitaji watu nane hadi 12 kutumia saa sita hadi nane pamoja na gharama ya ujira wa kati ya Sh. 40,000 hadi 60,000 kwa ekari, Rafiki Planter huokoa muda na fedha kwa kiwango kikubwa.

“Hii si tu mashine ya kupanda ni nyenzo ya kumkomboa mkulima na kumfanya awe mzalishaji wa kisasa. Ni mkombozi wa kilimo, hasa kwa vijana,” amesema.

Nyenzo Rahisi Ndio Kichocheo cha Vijana Kuingia Kwenye Kilimo

Amesema Serikali kupitia mpango wa ‘Building a Better Tomorrow’ (BBT) imekuwa ikihimiza vijana kushiriki katika kilimo cha kisasa lakini changamoto imekuwa zana duni lakini mashine hiyo imekuwa suluhisho.

Amesema Mkurugenzi wa Kituo cha TARI Ukirigulu, Dkt. Sabas Saidia ameshiriki kikamilifu katika utafiti na utengenezaji wa mashine hiyo pamoja na wataalamu wengine akiwemo Mtaalamu wa mbegu kituoni hapo, Robert Cheleo.

Amesema baada ya kufanyiwa majaribio katika mikoa ya Morogoro, Dodoma, Singida, Simiyu na Geita, mashine hiyo sasa ipo tayari kuingia sokoni.

“Maoni ya wakulima yamezingatiwa na maboresho kufanyika na sasa zaidi ya wakulima 50 wameonyesha nia ya kuinunua katika maonesho ya 49 ya biashara yanayoendelea.

“Kwa sasa, TARI imeingia makubaliano na Taasisi ya Usambazaji wa Zana Rahisi Vijijini (CAMATECH) kwa ajili ya kuzalisha mashine hizo kwa wingi na kuzisambaza nchini kote.

“Hii inaleta matumaini makubwa kwamba wakulima wengi wataweza kumudu teknolojia hiyo,” amesema.

Amesema Mpango wa Taifa wa kuhakikisha kilimo kinachangia angalau asilimia 10 ya pato la Taifa ifikapo mwaka 2030 unahitaji zana rahisi kama Rafiki Planter.

Hivyo ujio wa mashine hiyo ni ushahidi kwamba kwa uwekezaji sahihi kwenye ubunifu wa ndani, Tanzania inaweza kujitegemea kwenye mapinduzi ya kilimo.

“Tumeweza kutengeneza mashine moja, lakini haitoshi. Tunaomba serikali itusaidie kuzalisha mashine nyingi zaidi ili ziwafikie wakulima kwa wingi. Tukiwezeshwa, tuko tayari kwenda mbali zaidi – si kwa ndoto, bali kwa vitendo,” amesema.

Kwa sasa, timu hiyo ya wabunifu tayari ipo kwenye hatua za mwisho za kutengeneza toleo kubwa la mashine hiyo litakalokuwa na injini ya cc 300, yenye uwezo wa kulima hadi ekari 50 kwa siku – hatua inayokuza zaidi azma ya Tanzania kuwa Taifa la kilimo chenye tija.

You Might Also Like

Makala: Hakuna Kupita Bila Kupingwa

TRAWU Yazindua KAMPENI ya Afya Na Usalama Mahali Pa Kazi

UDSM Yamtunuku Rais AfDB Shahada Ya Heshima Ya Sayansi

Dkt. Bwana: Tunafanya utafiti wa mbegu kutatua changamoto za wakulima

TARI: Mabadiliko Ya Tabia Nchi Yamepunguza Ufanisi Wa Mbegu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wazalishaji, Waagizaji Mbolea Watakiwa Kuzingatia Afya ya Udongo kwa Tija ya Kilimo
Next Article UDSM  Yakamilisha Utafiti Wa Dawa Ya Kusafisha Sumu Kwenye Maji
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

BRELA Yatwaa Tuzo Sabasaba
Habari July 11, 2025
UDSM  Yakamilisha Utafiti Wa Dawa Ya Kusafisha Sumu Kwenye Maji
Habari July 11, 2025
Wazalishaji, Waagizaji Mbolea Watakiwa Kuzingatia Afya ya Udongo kwa Tija ya Kilimo
Habari July 11, 2025
Tanzania, Comoro Zaongeza Ushirikiano wa Lugha
Habari July 10, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?