-
Na Lucy Lyatuu,DodomaMAMLAKA ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA), imesema katika kipindi cha Uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imezuia utoaji wa tuzo za zabuni 43 zenye thamani ya sh milioni 586.5 kwa wazabini waliokosa iwezo wa kifedha na sifa za kitaalamu zinazohitajika kutekeleza zabuni husika.Mkurugenzi Mkuu wa PPAA,James Sando amesema hayo Leo na kuongeza kuwa hatua hiyo imezuia utekelezaji usioridhisha wa miradi ambao ungesababisha upotevu wa fedha za umma na kuchelewesha maendeleo mendelevium na stahiki kwa Wananchi.Amesema serikali inaamini kuwa usuluhishi wa migogoro hauwezi kufanikishwa katika mazingira ya ubaguzi Wala pale ambapo fursa na haki za kiuchumi na kiraia hazitokani kwa usawa.“Kwa hio hatua ya PPAA kuzuia utoaji wa tuzo kwa wazabini 43 waliokosa sifa za kutekeleza zabuni inaimarisha mchakato wa usuluhishi wa migogoro,” amesema.Ameongeza kuwa Mamlaka imeendelea kutekeleza azma ya Serikali ya kuwawezesha vijana na makundi maalum kwa kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo vijana 878 katika mikoa ya Dodoma, Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya ili waweze kudai haki zao kwa ufanisi katika michakato ya ununuzi wa umma.Amesema mafunzo hayo yamelenga kuwaimarisha vijana ili washiriki kikamilifu katika zabuni za umma na kufahamu taratibu sahihi za kuwasilisha malalamiko au rufaa wanapokumbana na changamoto.Hatua hivyo ametoa wito kwa wazabuni wote nchini pamoja na wadau wa ununuzi wa umma kujitokeza kushiriki mafunzo ya matumizi ya moduli ya kuwasilisha malalamiko na rufaa pindi Mamlaka inapoyatangaza.Amesema mafunzo hayo yatawawezesha kuelewa kwa undani namna ya kutumia moduli hiyo kwa usahihi na ufanisi.Kadhalika amebainisha kuwa kupitia moduli ya kuwasilisha malalamiko na rufaa katika mfumo wa NeST, Mamlaka ya Rufani imeunganisha taasisi zote za ununuzi nchini, hatua inayomwezesha mzabuni kuwasilisha rufaa yake kwa njia ya kielektroniki katika taasisi husika.Aidha, Mamlaka ina uwezo wa kufuatilia na kuona nyaraka zote zinazotumika katika mchakato wa zabuni inayolalamikiwa, jambo linaloongeza uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika ununuzi wa umma.

