MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Majaliwa: Serikali Yaanzisha Program Ya Uanagenzi Kwa Vijana
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Majaliwa: Serikali Yaanzisha Program Ya Uanagenzi Kwa Vijana
Habari

Majaliwa: Serikali Yaanzisha Program Ya Uanagenzi Kwa Vijana

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
MBEYA: WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema serikali imeanzisha programu maalum ya uanagenzi kupitia ofisi yake, inayolenga kuwapatia vijana wa Kitanzania ujuzi wa kazi bila kujali kiwango chao cha elimu.
Akizungumza katika maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Vijana yanayoendelea mkoani Mbeya, Majaliwa amesema programu hiyo inalenga vijana wote, hususan walioko katika mazingira magumu, ili kuwawezesha kujiajiri na kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo.
Amesema vijana wote wana nafasi ya kushiriki kwenye mpango huo ambapo serikali inawalipia ada kwa miezi sita wanapokuwa vyuoni, na baada ya kuhitimu wanaweza kujiajiri, kuajiri wengine au kuanzisha vikundi vya uzalishaji mali.
Habari Picha 9904
Vijana hao wanapatiwa mafunzo ya stadi mbalimbali zinazochochea uchumi na ajira, ikiwemo ufundi wa magari, umeme, kompyuta, uchomeleaji, usindikaji na ufungashaji wa vyakula, ususi, urembo na ushonaji.
Kwa mujibu wa Waziri Mkuu, tangu kuanzishwa kwa programu hiyo mwaka 2022 hadi 2025, jumla ya vijana 77,228 wamepatiwa mafunzo katika vyuo mbalimbali nchini.
Majaliwa amesema maadhimisho ya Wiki ya Vijana ni sehemu ya Siku ya Kimataifa ya Vijana inayotambuliwa duniani kote. Lengo lake ni kutoa fursa kwa vijana kujadili mafanikio, changamoto na nafasi yao katika kutimiza malengo ya maendeleo ya milenia.
Aliwahimiza vijana kuitumia siku hiyo kueleza changamoto wanazokabiliana nazo ili serikali iweze kuzifanyia kazi kwa ufanisi.
Pia amesema Serikali imefanya maboresho ya Sera ya Maendeleo ya Vijana ya mwaka 2017 na sasa inatekeleza sera mpya ya mwaka 2024, inayolenga kuboresha maisha ya vijana kwa kushirikiana nao pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo.
Vile vile imeimarisha programu ya uwezeshaji wananchi kiuchumi na kutoa elimu ya ujuzi bila malipo. Kwa upande wa elimu ya juu, serikali hutoa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu, huku vyuo vya elimu ya kati na ufundi stadi vikiimarishwa kwa lengo la kuwaandaa vijana kuingia kwenye soko la ajira kwa ufanisi zaidi.
Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Ridhiwani Kikwete, amesema maadhimisho ya kila mwaka ya Wiki ya Vijana ni jukwaa la kuwaunganisha wadau wa maendeleo kutathmini mchango wa vijana katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Ameongeza kuwa ni fursa pia ya kuwaenzi waasisi wa taifa, akiwemo Mwalimu Julius Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume, waliokuwa katika umri wa ujana walipokuwa wakiongoza harakati za ukombozi wa Afrika.

You Might Also Like

TARURA yaimarisha ubora wa barabara kwa kuwa na maabara mikoani

Elimu ya Ufundi Yachangia Maendeleo ya Taifa – VETA

Rafiki Planter’Teknolojia Rahisi, Tija Kubwa”

Maadhimisho Ya VETA Ya Miaka 30 Kuhitimishwa Machi 18 Hadi 21, DSM

Rais Mpya CWT Ikomba: ‘Nataka Kuwaunganisha Walimu, Kuitendea Haki Kazi Yetu’

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Zimamoto Mbeya Watoa Elimu Ya Kukabiliana Na Majanga Ya Moto Kwenye Wiki Ya Vijana
Next Article Wanawake 1,063 Wahitimu Mafunzo Ya Ujuzi VETA Mbeya Kupitia Mpango Wa Rais Samia
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?