MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Majaliwa Asisitiza Matumizi ya Mifumo ya Kieletroniki Katika Makusanyo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Majaliwa Asisitiza Matumizi ya Mifumo ya Kieletroniki Katika Makusanyo
Habari

Majaliwa Asisitiza Matumizi ya Mifumo ya Kieletroniki Katika Makusanyo

Author
By Author
Share
2 Min Read
– Awataka watumishi wa Umma Kuwatembelea Wananchi Walipo
Na Mwandishi Wetu
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amewataka Maofisa masuhuli kwenye Halmashauri nchini kuweka msisitizo wa kutumia mifumo ya kielektroniki katika makusanyo badala la kukusanya kwa fedha taslimu.
Majaliwa amesema kufanya hivyo kutasaidia kuongeza mapato katika maeneo yao na kuepuka vishawishi vya kutumia vibaya fedha za umma ambazo zinakusanywa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
Amesema hayo leo Oktoba 05, 2024 alipozungumza  na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke Mkoani Dar es Salaam.
“Suala la mapato ni lazima mliwekee msisitizo ili tupate matokeo mazuri kwenye halmashauri zetu,” amesema.
Pia ametoa wito kwa wakurugenzi wa Halmashauri kutumia mapato ya ndani katika kutekeleza miradi ya maendeleo badala ya kusubiri fedha kutoka Serikali kuu pekee.
“Acheni kutegemea mapato ya Serikali kuu pekee, tunataka kuona mapato ya ndani yanatumika katika kutekeleza miradi ya maendeleo.,” amesema.
Amewataka watumishi wa umma kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na uaminifu ili mipango na malengo ya Serikali ya kuwahudumia Watanzania yaweze kutimia.
Majaliwa amesema  watumishi wa umma ni wahudumu wa wananchi hivyo wanapaswa kuwahudumia ipasavyo kwenye maeneo yao na kutatua kero zao.
“Sisi tunataka tuone mkifanya kazi kwa bidii, uadilifu, uaminifu usipofanya hivyo utakuwa unakosa sifa za kuwa mtumishi wa umma.
“Sisi ni watumishi wa umma na ni wahudumu wa Wananchi, tumefunga mikataba ili tuwe wahudumu wao, tumekubali hilo, twende tukafanye kazi, tunapaswa kuwatembelea walipo, kila mmoja ana wajibu wa kuwahudumia wananchi kwenye maeneo yao,” amesema.

You Might Also Like

Serikali Yaja Na Kanuni Mpya Ya Sheria Ya Fidia   Kuboresha Mazingira Ya Mfanyakazi 

Afrika ijadili changamoto sekta ya utalii – UN

Rais Samia azindua bwawa la umwagiliaji Mtibwa

Wananchi Washauriwa Kujiunga Na Chuo Cha Ualimu Na Ufundi Stadi Morogoro

Kamati Ya Bunge Ya Ustawi Na Maendeleo ya Jamii, Yaipongeza Serikali Uwekezaji Kiwanda Cha Chai

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mbunge Kuchauka azindua kambi kuhamasisha Uchaguzi Serikali za  Mitaa
Next Article Masauni Kuzifanyia Kazi Changamoto Alizozibaini Katika Ziara Yake
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tume ya Kurekebisha Sheria Yaelimisha Umma Kuhusu Haki za Wanyama
Habari August 6, 2025
Bundi Wasaidia Kupambana na Panya: Teknolojia Asilia Inayobadili Maisha ya Wakulima
Habari August 6, 2025
Ofisa wa TARI Kuwapo Kila Kituo cha Umwagiliaji – Naibu Katibu Mkuu
Habari August 6, 2025
Mbinu Mpya za Kilimo kwa Vijana Zapata Umaarufu Nanenane Banda La VETA
Habari August 6, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?