MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Madaktari Toka China Waleta Matumaini Barani Afrika
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Makala > Madaktari Toka China Waleta Matumaini Barani Afrika
Makala

Madaktari Toka China Waleta Matumaini Barani Afrika

Author
By Author
Share
5 Min Read

Na Waandishi Wetu

TEKNOLOJIA ya ubunifu kutoka nchini China imewezesha ufanikishaji wa upasuaji wa kisasa usiohitaji kufungua kifua kwa watoto waliokuwa na matatizo ya moyo tangia walipozaliwa.

Ubunifu huo uliripotiwa na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) jijini Dar es Salaam iliyopo nchini Tanzania katika siku za karibuni baada ya watoto watano kufanyiwa upasuaji huo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyom upasuaji huo ulifanywa na timu ya pamoja ya madaktari wa China na Tanzania kwa kutumia teknolojia ya ubunifu kutoka China.

Kwamba, Mbinu hiyo ya upasuaji wa ndani kwa kutumia mwongozo wa mawimbi ya sauti, ilibuniwa na Profesa Pan Xiangbin na timu yake kutoka Hospitali ya Fu Wai,

Teknolojia hiyo, huondoa hitaji la kufungua kifua, huepusha madhara ya mionzi, hupunguza kwa kiasi kikubwa gharama za matibabu, na inaweza kufanyika hata katika maeneo ya mbali kwa kutumia magari maalum ya huduma ya matibabu inayotembea.

Kwa kutumia teknolojia hiyo inatoa matumaini ya maisha yenye afya bora kwa watoto wenye umri kati ya miaka mitatu hadi saba.

Mkurugenzi Mkuu wa JKCI, Dkt. Peter Kisenge ameeleza ikiwa teknolojia hiyo itasambazwa kwa kiwango kikubwa, idadi ya upasuaji kwa mwaka inaweza kuongezeka kutoka kwa wagonjwa 783 hadi zaidi ya 2,000.

Amesema teknolojia hiyo itakuwa hatua muhimu katika kuinua ubora na kiwango cha ushirikiano wa kitabibu kati ya China na Tanzania.

Tangu miaka ya 1960 nchi ya China imekuwa ikitoa msaada wa kitabibu Barani Afrika na imeandika historia yenye mafanikio makubwa nchini Tanzania.

Jumla ya timu 27 za madaktari zimefika Tanzania Bara, na nyingine 33 visiwani Zanzibar, ambapo zimesaidia kutoa huduma kwa zaidi ya wagonjwa milioni 10. Zaidi ya mbinu 100 mpya za kitabibu ziliwasilishwa hadi Bara la Afrika.

Picha hii inaonyesha timu ya madaktari kutoka China ikifanya kliniki ya kuhamahama mnamo Aprili 2025 katika mkoa wa Arusha, Tanzania.

Kwa mujibu wa huduma zinazotolea na China nchini Tanzania, moja ya mafanikio ya kihistoria ni Mradi wa Kudhibiti na Kuzuia Ugonjwa wa Kichocho ulioanzishwa Zanzibar mwaka 2017.

Kwamba kupitia mradi huo timu ya wataalamu kutoka China ilisaidia kupunguza kiwango cha maambukizi kutoka asilimia 8.92 hadi asilimia 0.64.

Kwa kutambua mchango huo wa kipekee, Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, aliwatunukia wataalamu hao medali za heshima mnamo Agosti mwaka jana, 2024.

Timu ya madaktari kutoka China inaongozwa na falsafa ya ‘Afadhali kumfundisha mtu jinsi ya kuvua samaki kuliko kumpa samaki’ inasisitiza uendelevu wa huduma za afya kwa njia ya mafunzo kwa wataalamu wa ndani na uhamishaji wa teknolojia za kisasa.

Lengo kuu ni kusaidia Tanzania kuinua kiwango cha huduma zake za afya kwa msingi wa kujitegemea.

Hivyo Kwa zaidi ya miaka 60 msaada wa kitabibu wa China Barani Afrika umekuwa mfano bora wa ushirikiano wa afya kati ya pande hizo mbili.

Zaidi ya madaktari 25,000 wa China wametumwa katika nchi 48 za Afrika, wakichangia kikamilifu katika utekelezaji wa mpango wa ‘Njia ya Ushirikiano wa Kiafya’.

Chini ya mwongozo wa dhana ya kujenga kwa pamoja Jumuiya ya Afya ya Binadamu timu ya madaktari wa China itaendelea kushikilia moyo wa ‘kutojali hatari na kushikilia moyo wa kujitolea’, ikiendelea kushirikisha uzoefu wao wa kuzuia na kudhibiti magonjwa, kubuni mbinu mpya za ushirikiano wa kitabibu, na kutoa msukumo wa kudumu wa kuimarisha uimara wa mifumo ya afya ya umma barani Afrika,

Pia kuinua afya na ustawi wa watu wake, na kuendelea kuandika sura mpya ya ushirikiano wa kujenga kwa pamoja Jumuiya ya China – Afrika yenye Mustakabali wa Pamoja.

Chini ya mwongozo wa dhana ya kujenga kwa pamoja Jumuiya ya Afya ya Binadamu, timu ya madaktari wa China itaendelea kuonyesha moyo wa dhati, kujitolea, na mshikamano.

Kwa kushirikiana uzoefu katika kuzuia na kudhibiti magonjwa, na kubuni mbinu bunifu za ushirikiano wa afya, wataendelea kuchangia katika kuimarisha ujenzi wa mfumo wa afya ya umma barani Afrika, kuinua viwango vya huduma za afya katika nchi za Afrika, na kufungua sura mpya ya Jumuiya ya China – Afrika yenye Mustakabali wa Pamoja.

Mwandishi Song Yiting, mwanafunzi wa shahada ya pili kutoka Chuo Kikuu cha Taaluma za Kimataifa cha Shanghai (SISU).

Barua pepe:Yiting_Mo@126.com

Mwandishi Ning Yi, mwalimu wa Kiswahili kutoka Chuo Kikuu cha Taaluma za Kimataifa cha Shanghai (SISU).

Barua pepe:02706@shisu.edu.cn

You Might Also Like

Tujenge Jumuiya Yenye Mustakabali wa Pamoja kati ya China na Afrika – Wang Yi

Mazao Bora Ya Kilimo Kutoka Tanzania Yavutia China

Ndunguru: Mabadiliko Ya Tabianchi Yanachangia Kuwepo Kwa Magonjwa, Wadudu Kwenye Mazao

Mawasiliano Kati ya China, Afrika Juu Ya Mtazamo Wa Maandishi Ya Kifasihi

Kitabu cha Utamaduni na Maendeleo Nchini Tanzania, Chaimarisha Mawasiliano ya Kitamaduni Baina ya China, Tanzania

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Maziwa Kukuza Uchumi Wa Wafugaji
Next Article Akili Bandia Yachochea Ushirikiano Kati Ya China, Afrika
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mchumi Ajitosa Kuwania Ubunge Manyoni
Habari July 1, 2025
Msomi Wa Afya, Fatuma Atia Nia Jimbo la Dodoma Mjini
Habari July 1, 2025
Dkt. Mashimba Achukua Fomu Ya Kuwania Nafasi Ya Ubunge
Habari July 1, 2025
TPHPA, MUCE Wasaini Hati Ya Makubaliano Maeneo Yanayogusa Sayansi
Habari July 1, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?