Na Lucy Ngowi
DODOMA: ZAO la mkonge lina fursa nyingi ikiwemo utengenezaji wa gypsum, mapambo ya nyumbani na sehemu nyingine.
Mkuu wa Sehemu ya Masoko na Uhamasishaji wa Bodi ya Mkonge Tanzania, David Maghali amesema hayo wakati wa maonesho ya wakulima, wafugaji na wavuvi yanaoendelea jijini Dodoma.
Amesema kutokana ukweli huo,wananchi wanapaswa kuchangamkia fursa hiyo kwa kulima zao la mkonge kwani maeneo ya kulima na masoko ni mengi.
Ameaema kwa sasa wateja wa zao hilo ni nchi za Afrika Magharibi kama Nigeria,,Ghana,Morocco,Saud Arabia na Misri ambao hutumia kutengeneza bidhaa za ujenzi kama gypsum na mapambambo huku Tanzania nayo ikiwa imeanza utumiaji wa teknolojia hiyo.
“Sekta ya mkonge ina fursa nyingi ambazo watu wanaweza kujiunga nazo,fursa namba moja ni wakulima kujiunga na kilimo cha mkonge ,mahitaji ya mkonge bado nni makubwa sana duniani lakini uzalishaji wake bado ni mdogo,
“Kwa kuwa sisi watanzania bado tuna maeneo ambayo hayatumiki kwa chochote wala hayana uzalishaji,tunawahimiza serikali kupitia Halmashauri kutenga maeneo kwa ajili ya kilimo cha mkonge ili kuinua wananchi wao kiuchumi lakini pia Bodi ya mkonge inaratibu masuala mbalimbali yahusuyo mkonge ,
“Kwa hiyo kwetu sisi mkonge siyo tatizo bali tunahitaji uratibu wa maeneo ya watanzania kufanya kilimo hiki,uwezo wa kufanya upatikanaji wa mashine kwa wakulima katika maeneo mwisho wa siku tutakuja kuratibu upatikanaji wa masoko aua uuzaji wa mkonge utakaokuwa umezalishwa,” amesema.
Kwa upande mwingine amesema zao hilo lina bei nzuri kwani kwa sasa tani moja ya mkonge inauzwa kwa sh milioni 3.9 wakati miaka mitano iliyopita iliuzwa kwa sh milioni 2.5 .
Amewahakikishia wakulima kuwa,zao hilo lina uhakika wa kuvuna na kuuza.