MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kitabu cha Utamaduni na Maendeleo Nchini Tanzania, Chaimarisha Mawasiliano ya Kitamaduni Baina ya China, Tanzania
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Makala > Kitabu cha Utamaduni na Maendeleo Nchini Tanzania, Chaimarisha Mawasiliano ya Kitamaduni Baina ya China, Tanzania
Makala

Kitabu cha Utamaduni na Maendeleo Nchini Tanzania, Chaimarisha Mawasiliano ya Kitamaduni Baina ya China, Tanzania

Author
By Author
Share
6 Min Read

Na Waandishi Wetu

KITABU cha Utamaduni na Maendeleo Nchini Tanzania, kilichotafsiriwa na walimu wa Kiswahili kutoka Chuo Kikuu cha Taaluma za Kimataifa cha Shanghai (SISU), kimetolewa nchini China.

Walimu waliotafsiri kitabu hicho wa nchini China ni Ma Jun na Ning Yi.

Kutokana na umahiri wake katika kutafsiri, kimewavutia wasomi wengi nchini China.

Hivyo kuwa kivutio katika nchi hiyo, kitabu hicho kimechaguliwa kuwa kimojawapo kati ya vitabu vinavyopendekezwa kwenye Orodha ya Kujumuisha Vitabu vya Kutafsiriwa Mwaka 2024, nchini China.

Tangu ianzishwe orodha ya kuwa na vitabu vilivyotafsiriwa mwaka 2018, kumekuwa na utaratibu wa kupendekeza vitabu vizuri kutafsiriwa kutoka lugha za kigeni kwenda lugha ya Kichina.

Orodha hiyo ya vitabu huchapishwa na Shirika la Uchapishaji wa Sayansi ya Kijamii, hutungwa na kutolewa mara kwa mara, ili kupendekeza kazi za kina na za kuvutia zilizotafsiriwa kwa wasomaji.

Mwaka 2024 ni maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na Tanzania.

Urafiki kati ya nchi hizi mbili una historia ndefu. Kitabu cha Utamaduni na Maendeleo Nchini Tanzania kiliandikwa na mwandishi Dkt. Daniel K. Ndagala, kamishna mstaafu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ya Tanzania.

Katika kitabu hicho Dkt. Ndagala amechambua kwa kina kuhusu uhusiano wa kitamaduni na mawasiliano ya kijamii kwa kuzingatia hali halisi ya Tanzania.

Kitabu hicho kinafafanua jukumu muhimu la utamaduni katika ujenzi wa taifa la Tanzania na maendeleo ya jamii, pia kinatoa mapendekezo ya ujumla kuhusu kutekelezwa kwa sera ya utamaduni.

Hivyo kinatoa suluhu kwa ajili ya ustawi wa utamaduni wa Tanzania na kuonyesha mfano bora kwa nchi nyingine zinazoendelea.

Kwa kulinganisha nadharia na uchanganuzi wa kesi halisi, kitabu hicho kinaeleza kwa kina historia na mabadiliko ya sera za utamaduni na miongozo ya maendeleo nchini Tanzania,

Pia kinatoa fursa kwa ulimwengu ili kuelewa sera za utamaduni na maendeleo ya kitamaduni ya serikali nchini Tanzania.

Dkt. Ndagala ni mtafiti, mwandishi na mshauri wa serikali ambaye anazingatia masuala ya utamaduni na maendeleo nchini Tanzania.

Amechapisha vitabu vitatu na tasnifu kadhaa kuhusu utamaduni na sera za utamaduni za Afrika. Anazingatia muingiliano kati ya sera za serikali na jamii za vijijini.

Walimu Ma Jun na Ning Yi, waliotafsiri kitabu hicho wanafundisha Kiswahili katika Chuo Kikuu cha SISU, pia katika Taasisi ya Taaluma za Afrika Mashariki ya SISU.

Tangu kuasisiwa kwake mwaka 2018, taasisi hiyo imefanya utafiti wa kina katika nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii na kitamaduni za nchi za Afrika Mashariki, huku ikiwakuza wanafunzi wengi wanaojua Kiswahili na utamaduni wa waswahili.

Rais Xi Jinping alitoa hotuba yake kwenye Mikutano ya Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) iliyofanyika Beijing mwaka 2024.

Kwenye hotuba hiyo, alisema baada ya juhudi za pamoja za miaka 70, uhusiano kati ya China na Afrika umeingia hatua bora zaidi kihistoria.

Rais Xi alipendekeza kuimarisha zaidi uhusiano kati ya China na Afrika, na kujenga kwa pamoja Jumuiya ya China-Afrika yenye Mustakabali wa Pamoja.

China na Afrika zinaafikiana katika kupata maendeleo na kukuza mambo ya kisasa.

Kuhusu mikakati ya kujenga na kudumisha amani, Mwandishi ametaja mila za utani katika sura ya mwisho ya kitabu hicho.

Utani ni uhusiano wa kindugu ulioko kati ya watu wa makabila mbalimbali ya Tanzania ambao unatokana na watu wa makabila hayo kuwa na uhusiano wa kivita, kibiashara na kadhalika.

Kwa kifupi, utani ni utamaduni wa amani wa makabila ya kibantu ya Tanzania, kwani kwa maoni ya mwandishi utani baina ya makabila ni mchango mkubwa wa watanzania katika dhana ya udumishaji wa utamaduni wa amani katika dunia.

Hivyo inahitajika utafiti zaidi ufanywe kuhusu Utani ili kuona jinsi ya kuendeleza falsafa hiyo kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Katika makala hii, Mwalimu wa lugha ya Kiswahili kutoka SISU, Ning Yi anasema kuchapishwa kwa Utamaduni na Maendeleo Nchini Tanzania kunatoa maudhui mengi ya kina kwa mawasiliano ya kitamaduni baina ya China na Tanzania.

Vile vile kunatia nguvu mpya katika mawasiliano ya kitamaduni baina ya China na Afrika.

Kitabu hicho kinarejea Tanzania kama mlango katika kufichua tamaduni tofauti na mchakato wa maendeleo ya jamii Barani Afrika.

Pia kinasaidia wachina kuelewa Afrika kwa mapana zaidi.

Vile vile mapendekezo ya ujumla ya kutekelezwa kwa sera za utamaduni katika kitabu hiki yanatoa mawazo na njia mpya kwa mawasiliano ya kitamaduni baina ya China na Afrika.

Mwandishi Song Yiting, Mwanafunzi wa Shahada ya Pili kutoka Chuo Kikuu cha Taaluma za Kimataifa cha Shanghai (SISU).

Barua pepe:Yiting_Mo@126.com

{

Mwandishi Ning Yi ni mwalimu wa Kiswahili kutoka Chuo Kikuu cha Taaluma za Kimataifa cha Shanghai (SISU).

Barua pepe:02706@shisu.edu.cn

 

You Might Also Like

BAADHI YA MATUKIO MAKUBWA YA UKATILI YALIYOFANYIKA MWAKA 2024

OSHA yaelimisha sheria mahala pa kazi kwa JOWUTA

MATUKIO YA MISIBA KWA WATU MAARUFU YALIYOJIRI KUANZIA JANUARI 2024, HADI DISEMBA 2024

Rais Samia ametekeleza kwa vitendo falsafa ‘kazi iendelee’

MATUKIO YALIYOJIRI KUANZIA JANUARI 2024, HADI SASA DISEMBA 2024:

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Kimwaga Mwenyekiti Mpya DCPC, Ahimiza Nidhamu
Next Article Rais Samia ametekeleza kwa vitendo falsafa ‘kazi iendelee’
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

JAB Yatoa Mwezi Moja Kuthibitishwa, kupewa vitabulisho
Habari May 22, 2025
Hali Ya Ulinzi Na Usalama Wa Mipaka Ni Salama
Habari May 22, 2025
Ulega Ataka Ushirikiano Miradi Ya Kimkakati Ikamilike Kwa Wakati
Habari May 22, 2025
Aloe Dorotheae, Mmea Unaopatikana Tanzania Pekee
Habari May 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?