MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Ushirikiano Wa Afrika, China Kuonyesha Mwelekeo Maendeleo Ya Dunia
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Makala > Ushirikiano Wa Afrika, China Kuonyesha Mwelekeo Maendeleo Ya Dunia
Makala

Ushirikiano Wa Afrika, China Kuonyesha Mwelekeo Maendeleo Ya Dunia

Author
By Author
Share
4 Min Read
Na Waandishi Wetu
UTOZAJI kodi ya juu umechochea migogoro ya kibiashara duniani, jambo hilo limejitokeza katika kipindi cha muhula wa pili kwa Rais wa Marekani Donald Trump.
Jambo hilo limechangia kuonekana kwa athari kwenye maeneo mbalimbali nchini Marekani.
Kwa kuwa thamani za hisa katika masoko ya fedha ya Marekani zilishuka, na sarafu ya dola na dhamana za serikali ya Marekani ziliuzwa kwa kiasi kikubwa kipindi fulani.
Kutokana na hali hiyo, Jumuiya ya wafanyabiashara ya Marekani inalalamika, upinzani wa kisiasa unaendelea, huku mbinu za serikali ya Marekani kushinikiza nchi nyingine zikikumbana na vikwazo.
Afrika ni miongoni mwa eneo lililoathirika kutokana na mvutano huo wa ushuru wa forodha.
Marekani imeweka ushuru wa zaidi ya asilimia 10 kwa uchumi mdogo na nchi maskini zaidi.
Lesotho imelazimishwa kutozwa ushuru wa kiwango cha juu cha asilimia 50.
Kama moja ya nchi maskini zaidi, Lesotho zinauza zaidi ya nusu ya mavazi yake kwa Marekani.
Hivyo sera mpya za ushuru wa forodha za Marekani zitasababisha kuanguka kwa sekta yake ya usindikaji wa mavazi na idadi kubwa ya wafanyakazi kupoteza kazi.
Uchumi wa nchi za Afrika ni mdogo na una muundo wa kipekee, na uwezo wao wa kukabiliana na hatari ni dhaifu.
Ushuru mkubwa umezidi kiwango ambacho nchi za Afrika zinaweza kuvumilia.
Msomi kutoka nchini Tanzania,
Benedict Huruma Mwakabungu, anasema sera mpya za ushuru za Marekani sio tu zimekiuka kanuni husika za Shirika la Biashara Duniani(WTO), bali pia zimepuuza sheria za kimsingi za uchumi.
Pia kuzifanya gharama za kufanya biashara kati ya nchi za Afrika na Marekani zipande kwa kasi.
Ili kutatua changamoto hizi, anapendekeza makampuni ya Afrika kurekebisha mikakati yao kwa njia ya kuangalia masoko ya nchi nyingine kama China, na kutafuta fursa mpya za ushirikiano kwa kupanua masoko ya nje.
Mbali na kuongeza ushuru wa forodha, utawala wa Rais Trump umekatisha msaada wa mabilioni ya dola za kimarekani kwa Afrika, kwa kufunga Shirika la ‘Misaada la ‘Millenium Challenge Corporation’
na kusababisha miradi ya miundombinu nchini Niger, Msumbiji kusitishwa.
Vilevile, ulitishia kutosaini tena Mpango wa Ukuaji na Fursa wa Afrika ( AGOA) na kudhoofisha zaidi biashara ya nje ya Afrika.
Hivyo Nchi za Afrika zinapaswa kutegemea kikamilifu kazi za eneo la Biashara Huria Afrika, kuharakisha ushirikiano wa biashara ndani ya eneo hilo na kufungua masoko mapya, ili kujiondoa katika tatizo hilo.
Wachambuzi wa kisiasa wa Afrika Kusini wanaamini kuwa, kuimarika kwa uhusiano wa kiuchumi wa Afrika na mataifa mengine kutaifanya Marekani kuwa mbali zaidi na jamii ya kimataifa.
Wakati China inapozidisha ujenzi wa jumuiya ya binadamu yenye mustakabali wa pamoja na kufanya kazi na mataifa mengine kuendeleza mambo ya kisasa, Marekani inaanzisha vita vya ushuru na kusukuma nchi nyingi kuelekea upande mwingine.
Vitendo hivyo vya Marekani sio tu vinadhuru maslahi ya nchi nyingine, lakini pia vinaweza kuleta madhara kwa nchi hiyo.
Wakati huo huo, juhudi za nchi za Afrika za kuchunguza njia mpya za maendeleo zimebainisha kuwa ushirikiano wa kimataifa na faida ya pande zote ndio mwelekeo halisi wa maendeleo ya dunia.

Ning Yi, mwalimu wa Kiswahili kutoka Chuo Kikuu cha Taaluma za Kimataifa cha Shanghai (SISU).

Barua pepe:02706@shisu.edu.cn

  

                                        

Ye Tianfa, mwalimu wa Kiswahili kutoka Chuo Kikuu cha Lugha za Kigeni cha Tianjin (TFSU)

Barua pepe: tianfa202123@163.com

 

 

 

You Might Also Like

Dkt. Biteko Afuta Likizo Za Watumishi Wote Tanesco

MATUKIO YA MISIBA KWA WATU MAARUFU YALIYOJIRI KUANZIA JANUARI 2024, HADI DISEMBA 2024

Mafanikio Ya Veta Katika Kuadhimisha Miaka 30:

Tujenge Jumuiya Yenye Mustakabali wa Pamoja kati ya China na Afrika – Wang Yi

Shen Zhiying: Mkongwe Aliyeanzisha Kozi Ya Kiswahili Nchini China

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Ushirikiano Wanataalum, Wanatasnia Kisekta Ni Muhimu Katika Maendeleo Kiuchumi
Next Article LATRA Kuwapiga ‘Stop’ Wasiokamilisha Utaratibu, Tiketi Mtandao
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mfumo wa Usalama Majumbani, Umewakumbuka Wenye Ulemavu
Habari July 3, 2025
VETA Shinyanga Waja Na Mafunzo Ya Saluni, Mapambo, Urembo
Habari July 3, 2025
Tunapokea Malalamiko Ya Wananchi, Tunayafanyia Kazi – Dario
Habari July 2, 2025
VETA Mtwara Yawafundisha Wanafunzi Uongezaji Thamani Kwenye Korosho, Mwani
Habari July 2, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?